Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea kutoa elimu kwa Umma kuhusu mjukumu, malengo pamoja na mafanikio yake kupitia Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Kupitia maonesho ya Sabasaba yanayoendelea wananchi, wazabuni, taasisi nunuzi pamoja na wadau wa sekta ya ununuzi wameendelea kupata elimu kuhusu PPAA na majukumu yake.

Mapema leo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo TIB, Bi. Lilian Mbassy ametembelea banda la PPAA katika maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, Bi. Mbassy amepata fursa ya kuelezewa majukumu na malengo ya Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) kutoka kwa maafisa wa Mamlaka.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...