Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Felipe Nyusi amekutana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi Ikulu Zanzibar.

Akizungumza na Dkt. Mwinyi Mheshimiwa Nyusi alitumia nafasi hiyo kumuaga kwa kuwa amemaliza kipindi chake cha uongozi nchini Msumbiji na kumshukuru kwa Ushirikiano aliompatia alipokuwa Waziri wa Ulinzi wa Tanzania.

Amemuahidi kuwa Msumbiji itaendelea kudumisha uhusiano na ushirikiano wake na Tanzania haşa ikizingatiwa historia ya uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji

Naye Mhe. Dkt. Mwinyi amemshukuru Mhe. Nyusi kwa kumtembelea Zanzibar na kumkaribisha kutembelea Zanzibar wakati mwingine.

Mheshimiwa Nyusi alikuwa nchini kwa ziara ya kitaifa kuanzia tarehe Mosi Julai 2024.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...