NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS), Kanda ya Mashariki limeteketeza bidhaa hafifu tani 4.5 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 90 mara baada ya kufanya ukaguzi na kufanikiwa kukamata bidhaa hizo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo ambalo limefanyika leo Julai 5,2024 Pugu Jijini Dar es Salaam, Kaimu Meneja Kanda ya Mashariki, Francis Mapunda amesema kuwa walifanya oparesheni ya Ukaguzi Kanda ya Mashariki na kubaini kuwepo udanganyifu kwa baadhi ya wafanyabiashara kuuza bidhaa zilizo chini ya kiwango.

Amesema kuwa bidhaa hizo wamezikamata katika Mkoa wa Dar es Salaam, Morogoro na Pwani ambapo bidhaa hizo zilikuwa hazijasajiliwa, zilizoisha muda wa matumizi pamoja na bidhaa zisizosalama kwa walaji.

Aidha amewaonya wafanyabiashara wanaouza bidhaa zilizoisha muda wake ambapo amesema wanapaswa kuwa na utamaduni wa kukagua bidhaa zao na kama zimeisha muda wake ni vyema wakaziondoa mara moja ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza.

Pamoja na hayo amewaasa wananchi kuwa makini na ununuaji wa bidhaa sokoni ikiwemo chakula kuangalia tarehe ya za kutengenezwa na tarehe za kuisha muda wake lakini vilevile na kuangalia kwenye mitandao ya kijamii bidhaa ambazo zimepigwa marufuku kwamba si salama kwa matumizi ya binadamu.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...