· Kupitia kampeni hii, wateja wateweza kununua simu janja kwa mawakala waliodhinishwa na Samsung kupitia malipo nafuu ya mkopo ya kuanzia shilingi 1200 pekee kwa siku, wiki au mwezi kwa kipindi cha miezi 12.
· Lengo kuu la kampeni ya ‘Samsung Kibingwa’ ni kuwawezesha Watanzania ambao wanatumia simu za vitochi au analogia kuingia katika ulimwengu wa kisasa.




Meneja wa Mauzo ya Simu wa Samsung Tanzania, Baraka Siwa (wa kwanza kulia) akiwa timu ya mauzo na mabalozi wa kampuni hiyo wakati wa shughuli za kampeni ya ‘Samsung Kibingwa’ mkoani Morogoro.





Wakazi wa mkoani Tanga wakipata maelezo kutoka kwa miongoni mwa mabalozi wa Samsung Tanzania kuhusu kampeni ya ‘Samsung Kibingwa’ ambayo inawezesha kununua simujanja kwa mkopo nafuu.
Kampeni hiyo iliyozinduliwa mapema mwezi huu inalenga kuwawezesha wateja na Watanzania wote kwa ujumla kumiliki simu janja na kuachana na za analogia kupitia mikopo nafuu ambayo wanaweza kuilipa kwa siku, wiki, mwezi mpaka miezi 12.
Watanzania wanaweza kunufaika na kampeni hii, itakayofanyika nchi nzima, kwa kutembelea wauzaji walioidhinishwa na Samsung pamoja na maduka ya Watu Simu, mawakala, na ofisi zao ili kujipatia simu kama vile Samsung Galaxy A05, Galaxy A15, Samsung Galaxy A25 5G, Samsung Galaxy A35 5G, na Samsung Galaxy A55 5G.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...