Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni amepita Mtaa kwa Mtaa kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la mkazi ili waweze kuwa na sifa za kushiriki kuchagua Viongozi wa Serikali za Mitaa/Kitongoji Novemba 27 mwaka huu 2024.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo DC Kasilda amesisitiza wananchi ambao bado hawajajiandikisha kutumia vyema siku mbili zilizo baki kufika kwenye vituo kujiandikisha kwani Uchaguzi huu unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu ni muhimu kwa ustawi wa Taifa na ndiyo unatoa dira ya Uchaguzi mkuu wa mwakani 2025 wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Aidha amesema Wilaya ya Same ina Vitongoji 503 ambapo kila Kitongoji ni Kituo cha kujiandikisha na jambo la muhimu ni mwananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la mkazi linalofanyika kwa muda wa siku kumi kuanzia Oktoba 11 hadi 20.

Pia amesisitiza kuwa kitamburisho cha mpiga kura kinachotolewa na tume ni kwaajili ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ambao utafanyika mwakani 2025. hivyo kwa Uchaguzi huu ili mwananchi uweze kupiga kura kuchagua viongozi wa Mtaa/Kitongoji chako lazima ujiandikishe kwenye daftari la mkazi.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...