Na Mwandishi Wetu
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira inayoongozwa na mwenyekiti
Jackson Kiswaga imepokea taarifa kuhusu matumizi ya mitambo ya kisasa 25 ya kuchimba visima.
Taarifa hiyo imetolewa Jijini Dodoma ambapo imehusu pia visima na hatua iliyo fikiwa katika usambazaji wa maji ya visima na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).
Mitambo hiyo ya kisasa ilitolewa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha huduma ya majisafi inaimarika nchini.
Taarifa kuhusu mitambo hiyo imeeleza namna inavyojenga weledi na ufanisi kwa wataalam pamoja na watendaji wengine katika kuongeza kasi ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini kwa kutumia teknolojia na vifaa vya kisasa
Mafanikio yaliyopatikana katika uchimbaji wa visima ni pamoja na kuchimba na kuendeleza idadi ya visima 650 katika vijiji 876 na kunufaisha zaidi ya wananchi milioni sita.





KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira inayoongozwa na mwenyekiti
Jackson Kiswaga imepokea taarifa kuhusu matumizi ya mitambo ya kisasa 25 ya kuchimba visima.
Taarifa hiyo imetolewa Jijini Dodoma ambapo imehusu pia visima na hatua iliyo fikiwa katika usambazaji wa maji ya visima na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).
Mitambo hiyo ya kisasa ilitolewa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha huduma ya majisafi inaimarika nchini.
Taarifa kuhusu mitambo hiyo imeeleza namna inavyojenga weledi na ufanisi kwa wataalam pamoja na watendaji wengine katika kuongeza kasi ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini kwa kutumia teknolojia na vifaa vya kisasa
Mafanikio yaliyopatikana katika uchimbaji wa visima ni pamoja na kuchimba na kuendeleza idadi ya visima 650 katika vijiji 876 na kunufaisha zaidi ya wananchi milioni sita.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...