KAIMU Katibu Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa Uvccm, Bulugu Magege, amekitaka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuacha kulinajisi zoezi la uandikishaji wa wapiga kura linaloendelea nchini.

Akizungumza leo, Septemba 16, Jijini Dodoma, alipojiandikisha katika shule ya Dodoma Mlimani, Burugu amewasihi vijana kujitokeza kwa wingi katika mchakato huu muhimu wa kujiandikisha na kupiga kura.

Amesema kitendo cha viongozi wa Chadema kuzuia vijana wenye umri wa miaka 18 kujiandikisha kinawanyima haki zao za msingi na kikatiba.

Amesisitiza kwamba zoezi hili linasimamiwa kwa umahiri na Tamisemi, akionyesha kuridhishwa na idadi kubwa ya vituo vya kujiandikisha vilivyowekwa.

Burugu ameongeza kuwa ni muhimu kwa vijana kutumia fursa hii ili kuweza kushiriki katika mchakato wa kidemokrasia na kuhakikisha sauti zao zinaskika.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...