Na Oscar Assenga,TANGA

MBUNGE wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu amesema kazi ya Rais Dkt Samia Suluhu anayoifanya ya Maendeleo katika Mkoa wa Tanga sio ya kutafuta kwa Tochi.

Ummy aliyasema hayo leo wakati akitoa salamu katika Kongamano la Samia Challenge 2024 ambalo limeandaliwa na African Anti-Violence Journalist lililofanyika Jijini Tanga kwenye ukumbi wa Samia Business Centre Kange.

Ambapo alisema kuna miradi mingi ya maendeleo ikiwemo ya Afya,Umeme,Elimu,Maji na Vitega Uchumi karibia kila kona ambayo imechangia kuinua uchumi wa mkoa wa Tanga.


Alisema kwa sababu katika kila eneo la maendeleo utamkuta Rais Samia na kubwa zaidi ambalo wanajivunia nalo ni maboresho makubwa ya Bandari ya Tanga ambapo uwekezaji uliofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu ni wa Bilioni 429.1

“Kutokana na hili sasa tunatembelea kifuata mbele kutokana na uwekezaji huo ambao umeufanya mkoa huo kuanza kupokea meli kubwa zinazoleta shehena za magari na hilo linaonyesha matunda ya uwekezaji katika Bandari kwa kuchimbwa kina na meli kutia nanga gatini “Alisema

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...