WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzani (TFS) umewataka watanzania kuchangamkia fursa ya Utalii wa Nyuki, kutumia sumu ya nyuki kama tiba mbadala ya magonjwa mbalimbali ya kuambukizwa na yasiyoambukizwa.
.jpeg)
Alisema tafiti zinaonesha kuwa sumu ya nyuki ina mchanganyiko wa kampaundi nyingi zilizotengenezwa na nyuki ambapo mwilini mwa binadamu inasaidia kumkinga na vimelea vya magonjwa mbalimbali.
Lisa Richard mkazi wa Mkoa wa Geita ambaye anafanya kazi Benki ya CRDB amesema hii ni mara ya 3 kufika Banda la Maliasili na kutumia Tiba hiyo ya kudungwa na Nyuki na amesema kwake inamsaidia kujikinga na maradhi na baada ya kutumia njia hiyo ya Tiba ya Nyuki atakuwa anafanya mara kwa mara peke yake kwa kuzingatia maelekezo ya wataalam wa ufugaji nyuki kwa kuwa elimu hiyo imemsaidia baada ya kufika katika Banda la Maliasili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...