
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani S. Jafo leo tarehe 31 Oktoba 2024 amemuwakilisha Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Soko Huru la Kusina na mashariki mwa Africa(COMESA).
Mkutano huo umefanyika katika Jiji la Bujumbura nchini Burundi ukilenga kuimarisha Mtengamano wa kikanda kupitia kuongeza thamani kwa kilimo himilivu kwa mabadiliko ya Tabianchi na thamani ya Madini,na kuimarisha Utalii.
Tanzania inashiriki mkutano huo kama waangalizi kwani Tanzania bado ipo katika Mchakato wa kikamilisha utatu wa EAC-SADC-COMESA.
Ushiriki wa Tanzania katika mkutano huo ni moja na kuongeza fursa ya nchi ya Tanzania katika masuala ya biashara na kujenga uchumi wa nchi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...