Na Pamela mollel, Arusha

Katika kukuza utalii hapa nchini,Zanzibar na Mkoa wa Arusha yaungana kukuza soko la utalii kimataifa na kutanua wigo kwenye eneo la Utalii wa Urithi,Utalii wa michezo na Utalii wa afya kupitia msimu wa kwanza wa Tamasha la Utalii na Uwekezaji Zanzibar utakaofanyika Oktoba 25-26 mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari,katibu Mtendaji Kamisheni ya Utalii Zanzibar Aris Abbas Manji,anasema ujio wao Arusha ni kutangaza Tamasha hilo la utalii na uwekezaji kwa wadau wote wa utalii ili waweze kushiriki katika Tamasha hilo

Ameongeza kuwa Uchumi wa Zanzibar umekuwa ukichangiwa na sekta ya utalii kwa asilimia thelasini ambapo wameweza kutanua wigo wa bidhaa za utalii

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Poul Makonda amepongeza ujio huo wa Tamasha la kwanza la utalii na uwekezaji Zanzibar,ambapo ameeleza kuwa Mkoa wa Arusha upo bega kwa bega na Zanzibar katika kuhakikisha wanachochea na kutengeneza mazingira mazuri katika sekta ya utalii ili kuwavutia Wageni wengi zaidi na kutoa ajira kwa vijana.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...