Tanzania na Shirikisho la Jamhuri ya Somalia zinatarajia kufanya mazungumzo yanayolenga kuibua maeneo mapya ya ushirikiano na kuongeza uhusiano wa kidiplomasia na uchumi yatakayofanyika jijini Mogadishu kuanzia tarehe 17 -19 Disemba 2024.

Ujumbe wa Tanzania tayari umeanza kuwasili nchini humo kushiriki katika vikao vya ngazi ya Wataalamu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano wa ngazi ya Mawaziri unaotarijiwa kufanyika tarehe 19 Disemba 2024.

Katika mazungumzo hayo Tanzania itawakilishwa na ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wizara ya Utalii, Wizara ya Afya na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Abdulle jijini Mogadishu, Shirikisho la Jamhuri ya Somalia

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akisalimiana na Balozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Somalia Mhe. Ilyas Ali Hassan alipowasili jijini Mogadishu tarehe 17 Disemba 2024.
Kikao cha ngazi ya Wataalamu kikiendelea 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...