Tanzania na Shirikisho la Jamhuri ya Somalia zinatarajia kufanya mazungumzo yanayolenga kuibua maeneo mapya ya ushirikiano na kuongeza uhusiano wa kidiplomasia na uchumi yatakayofanyika jijini Mogadishu kuanzia tarehe 17 -19 Disemba 2024.
Ujumbe wa Tanzania tayari umeanza kuwasili nchini humo kushiriki katika vikao vya ngazi ya Wataalamu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano wa ngazi ya Mawaziri unaotarijiwa kufanyika tarehe 19 Disemba 2024.
Katika mazungumzo hayo Tanzania itawakilishwa na ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wizara ya Utalii, Wizara ya Afya na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Ujumbe wa Tanzania tayari umeanza kuwasili nchini humo kushiriki katika vikao vya ngazi ya Wataalamu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano wa ngazi ya Mawaziri unaotarijiwa kufanyika tarehe 19 Disemba 2024.
Katika mazungumzo hayo Tanzania itawakilishwa na ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wizara ya Utalii, Wizara ya Afya na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...