Na Mwandishi wetu Dodoma


Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewahimiza wananchi kutumia msimu wa sikukuu na likizo kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kujifunza, kuburudika, na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma jana, Mkurugenzi wa Masoko wa TTB, Ernest Mwamwaja, alisema Tanzania imejaliwa kuwa na vivutio vya kipekee ambavyo vinapaswa kuthaminiwa na Watanzania wenyewe.

“Msimu huu wa sikukuu ni fursa muhimu kwa wananchi kutembelea vivutio vilivyopo nchini ili kujivunia urithi wetu wa asili na kiutamaduni,” alisema Mwamwaja.

Aliongeza kuwa, “Tulizindua kampeni maalumu ya kuhamasisha utalii wa ndani katika msimu huu wa sikukuu ijulikanayo kama ‘Funga Mwaka Kijanja Talii,’ inayolenga kuwahamasisha Watanzania wa rika zote kushiriki katika shughuli za utalii. Kampeni hii itakoma ifikapo Januari 10, 2024.”

Mwamwaja alisema TTB imejipanga kushirikiana na waandishi wa habari ili kuongeza idadi ya watalii, kwa lengo la kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya 2020-2025 inayolenga kufikia watalii milioni tano.

Aidha, alisema jitihada hizo pia zinaunga mkono juhudi za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kukuza sekta ya utalii na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

“Tunaamini kupitia waandishi wa habari tunaweza kuwafikia wananchi wengi zaidi na kutangaza vivutio vya utalii, ili kuongeza idadi ya watu wanaotembelea vivutio vyetu,” alisema Mwamwaja.

Alisisitiza kuwa ni muhimu wananchi kuchangamkia fursa ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo Nchini



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...