Waziri 
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud 
Thabit Kombo (Mb.) tarehe 16 Desemba, 2024 amewasili jijini Addis Ababa,
 Ethiopia kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 16 hadi 18 
Desemba, 2024 na kupokelewa na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
 nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo katika ofisi za ubalozi huo.
Baada
 ya kuwasili Mhe. Kombo alifanya kikao kazi na watumishi wa Ubalozi huo 
pamoja na Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa Kwanza wa Tume ya 
Pamoja ya Mawaziri (JMC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 
Jamhuri ya Shirikisho la Ethiopia unaotarajiwa kufanyika tarehe 17 
Desemba, 2024 jijini Addis Ababa.
Waziri Kombo anatarajiwa 
kuongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano huo wa
 JMC akiwa ameambatana na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa 
(Mb.) ambapo pamoja na masuala mengine mkutano huo unatarajiwa kujadili 
utekelezaji wa maeneo mbalimbali ya ushirikiano yaliyokubaliwa na nchi 
hizo mbili ikiwemo masuala ya ulinzi na usalama, diplomasia, afya, maji,
 elimu, fedha, mifugo na uvuvi, kilimo, biashara na uwekezaji, viwanda, 
nishati, ushiririkiano katika sekta ya anga na michezo, Sanaa na 
utamaduni.
Mkutano wa Mawaziri ulitanguliwa na Mkutano wa ngazi 
ya Maafisa Waandamizi uliofanyika tarehe 16 Desemba, 2024 ambapo ulikuwa
 na jukumu la kupitia nyaraka mbalimbali ikiwa ni sehemu ya maandalizi 
ya mkutano huo muhimu wenye lengo la kukuza ushirikiano wa kimaendeleo 
kwa maslahi ya pande zote mbili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


 





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...