Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo tarehe 22.01.2025 Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo amesema zawadi hizo zitatolewa kwa Walipakodi waliyofanya vizuri katika kulipa Kodi kwa kipindi cha Julai 2023 mpaka June 2024.
Kayombo ametaja vigezo walivyotumia kuwachagua wanaopewa zawadi ikiwemo Mlipakodi kodi mwenye rekodi nzuri katika ulipaji wa Kodi, Mlipakodi kwa hiari na kwa wakati, Mlipakodi anayetumia EFD mashine kikamilifu, Mlipakodi aliyelipa kodi kubwa zaidi na Mlipakodi anayetoa ushirikiano kwa TRA.
Kayombo amesema zawadi hizo zitachagiza Walipakodi wengine kufanya vizuri zaidi ili na wao watunukiwe wakati ujao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...