MBUNGE wa Jimbo la Morogoro mjini, Abdul Azizi Abood amelipongeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro kitengo cha usalama barabarani kwa kuratibu mafunzo ya udereva wa pikipiki na bajaji kwa vijana wasio na leseni katika Manispaa hiyo

Abood ametoa pongezi hizo leo Februari 11, 2025 wakati wa zoezi la utoaji vyeti lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kikosi cha Usalama barabarani mara baada ya mafunzo hayo kukamilika.

Kwa upande wake Mkuu wa usalama barabarani Mkoa wa Morogoro SP Gabriel Chiguma amesema, lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwapa ujuzi wa kuendesha vyombo vya moto na kuwapa uelewa juu ya sheria, alama na michoro ya usalama barabarani.

Akida Jumbe, dereva wa bajaji Manispaa ya Morogoro amesema mafunzo hayo yatamfanya asiogope tena Polisi wa usalma barabarani kwani itakuwa chachu kwake kufuata sheria kwa sababu amezifahamu.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...