MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es salaam iliyoketi katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi kisutu imemuhukumu mfanyabiashara, Khamis
Luwongo (45) kunyongwa hadi kufa baada ya kukutwa na hatia ya mauaji ya
aliyekuwa mke wake Naomi Marijani na kumchoma moto kwa kutumia magunia
mawili ya mkaa.
Awali,Luwongo alijaribu kuizuia Mahakama Kuu
Kanda ya Dar es Salaam kutomsomea adhabu yake hadi atakapozungumza yeye
hali hiyo ilisababisha taflani kati ya mshtakiwa na Jaji Hamidu Mwanga,
baada ya mshtakiwa kutaka kutumia mabavu kuzungumza anachokitaka yeye
baada ya wakili wake kumaliza kuiomba Mahakama ipunguzie adhabu mteja
wake.
Hukumu hiyo imetolewa Leo Februari 26,2025 na Jaji, Hamidu
Mwanga na kabla ya kutoa adhabu hiyo alitoa maelezo yaliyopelekea
mshitakiwa kukutwa na hatia katika kosa hilo.
Jaji Mwanga alisema
mshitakiwa alitia hatiani kwa kosa hilo kutokana na ushahidi uliotolewa
na mashihidi 14 pamoja na viellezo kikiwemo melezo ya onyo ambayo
mshitakiwa alichukuliwa akiwa katika kituo cha polisi.
Jaji
Mwanga amesema kuwa katika ushahidi uliotolewa ilidaiwa kuwa kulikuwa na
mgogoro wa muda mrefu kati ya Hamisi na mkewe Naomi na baadae marehemu
alidaiwa kupotea, katika kupotea huko Hamisi alitoa taarifa za
kutoonekana kwa mke wake ikiwemo katika vituo vya polisi.
Akiwa
anaendelea kufuatilia taarifa za mke wake Hamisi alidai kuwa alitumiwa
ujumbe kutoka kwa Naomi akimwambia kuwa aliamua kwenda nje ya nchi hivyo
alimtaka awe analea mtoto wao.
Ilidaiwa kuwa Julai 16,2019
katika kituo cha polisi cha kati wakati Hamisi akiwa anaendelea na
harakati za kutoa taarifa polisi juu ya maendeleo ya mke wake alihojiwa
kuhusu jumbe alizodaiwa kutumiwa na mke wake kwani kwa uchunguzi wa
kielektroniki ilionyedha kuwa jumbe hizo zilitumwa katika sehemu moja.
Aidh,
Jaji amesema ni jukumu la upande wa mashitaka kuthibitisha hatia ya
mshitakiwa na katika mauaji inatakiwa kuthibitishwa kama mtu kweli
amekufa na kifo chake kuwa sio cha kawaida.
Amesema katika kesi
kuna mazingira tofauti kidogo na mazingira yake yanaonyesha kuwa
hakukuwa na mwili kuthibitisha kuwa kweli Naomi amekufa na kama hakuna
mwili basi uchunguzi wa kitabibu haukufanyika kubaini marehemu alikufa
kwa sabbau au kutokana na nini.
Ameongeza kuwa kutokana na kesi
zilizothibitishwa kutoka nchini India zilionyedha kuwa kifo cha mtu
kinaweza kuthibitishwa kwa ushahidi wa mazingira ambayo kifo hicho
kimetokea na uchunguzi unaweza kufanyanyika pasipokuwa na mwili.
“Sio
lazima kuwe na mwili ikiwa ni suala la lazima kuwepo na mwili ili
kuthibitisha hatia tutawapa watu upenyo wa kuteketeza ili kukimbia
ushahidi,” amesema Jaji Mwanga.
Pia amesema kuwa katika mashahidi
hao wapo waliokwenda Morogoro na kwa upande wa mkemia alileta majibu
kuwa alishindwa majibu ya moja kwa moja kwani ilibainika mabaki
yaliyopatikana yalikuwa ni ya mwanamke lakini haikuthibitihshwa kuwa ni
ya Naomi .
Jaji Mwanga amesema kuwa katika maelezo ya onyo ya
Hamisi alidai kuwa mabaki yale ni ya ya Naomi na alidaiwa kuwa Naomi
amefariki na mshitakiwa ndiyo aliyemuua na pia chumba alichokuwa akilala
Naomi kilikutwa na mabaki ya damu na yalidaiwa kuwa ni ya Naomi.
Pia
kwa mujibu wa maelezo ya onyo ya mshitakiwa alidai kuwa Mei 14,2019 ni
siku ambayo hakulala nyumbani kwake kwani alilala kwa Margreth alirudi
kwake asubuhi na kumkuta mke wake akimuandaa mtoto kwenda shule alidai
alimpita bila kusema chochote na mtoto alichukuliwa na bodaboda
kupelekwa shule.
Aliendelea kudai kuwa simu iliita kwa jina la
Magreth ndipo Naomi alianza kumtukana na Hamisi akamwambia achukue
chochote anachokitaka kwani hakukuwa na ndoa tena kati yao wakati wa
ugomvi Naomi alidondoka chini na kujigonga kichwani na damu zikaanza
kutoka akawa analalamika akitetemeka sitomsamehe.
Baadaye alianza
kukoroma hadi umauti ulipomfika baada ya Naomi kufa Hamisi akataka
kuundoa mwili ndipo alipouzungusha kwenye shuka mbili na baada ya kuona
kuwa akitoka na mwili ule kwenye gari akiwa barabarani askari
wangemsimamisha na kuuona ndipo alipokumbuka katika banda la kuku
kulikuwa na shimo kwa ajili ya kupitisha maji.
Alipokumbuka hili
alichukua mwili na kwenda kuuchoma na magunia mawili ya mkaa ili uungue
taratibu kwani alihofia kuchoma na kuni zingekuwa nyingi na wakati mwili
ulipoungua na kubaki mkaa alimtuma bodaboda kwenda kununua mafuta na
alipofiki alikwenda kuyachukulia getini ili asiingie ndani.
Pia
jaji aliendelea kusema kuwa maelezo hayo yanaeleza kuwa kwakuwa mafuta
ya taa yangeisha haraka akachukua viatu na kuviweka ili uendelee kuungua
taratibu na baada ya hapo alichukua mabaki na majivu na kupanda gari
yake aina ya Subaru na kuondoka hadi shambani kwake Morogoro ndipo
alipofukia na kupanda Mgomba juu ya mabaki hayo.
Jaji amesema
hakuna mtu anayeweza kutoa mtiririko huo wa matukio isipokuwa tu yule
anayejua ukweli wa tukio hilolilivyotokea, hivyo alisema kuwa maelezo
hayo ni ya kweli na ya kuaminika.
Pia amesema kuwa ushahidi
uliotolewa na shahidi namba nne ambaye alikuwa ni Mpwa wake ni wa
kuaminika kwani hakuwa na sababu ya kumuongelea uongo mjomba wake kwa
sababu ndiye aliyemtoa kijijini kumleta Dar es salaam kwa ajili ya
kufanya kazi.
"Kwenye maelezo haya ya onyo mshtakiwa anaeleza
vizuri sana hadi alivyochukua laini za mke wake akaanza kujitumia ujumbe
mfupi na pia amesema alitoa taarifa kwa ndugu wa marehemu kuwa Naomi
amesafiri nje ya nchi," amesema Jaji Mwanga
Baada ya
mshitakiwa kukutwana hatia alipata nafasi ya kujitetea na katika utetezi
wake alidai kuwa maelezo hayo ya onyo yalikuwa si ya kwake na jaji
alisema mahakama ilitupilia mbali kwani hakukataa maelezo hayo mara ya
kwanza yalipoletwa kama kilelezo mahakamani.
Amesema pia mahakama
inaangalia baada ya mauaji ni kitu gani kilitendeka na kwa mujibu wa
maelezo maada ya mauaji aliviringisha mwili kwenye shuka mbili na kwenda
kuuchoma na kwa mujibu wa maelezo hayo inaonyesha mshitakiwa
alidhamiria kutenda kosa.
Pia mawakili wa mshitakiwa walidai kuwa
mshitakiwa alitenda kosa akiwa hana akili timamu na alichukuliwa na
kupimwa uwezo wake wa kufikiri lakini kutokana na mtiririrko
ulivyojieleza mshitakiwa alionekana kuwa na akili timamu kwani aliweza
kufikiria kutenda matukio yote.
Jaji alisema kuwa mahakama hiyo
ilimtia hatiani mshitakiwa kwa kumuua mke wake chini ya kifungu namba
196 na 197 cha sheria ya adhabu.
Wakili wa Serikali Mwandamizi,
Ashura Mzava alieleza mahakama kuwa mshitakiwa hana rekodi ya makosa ya
nyuma lakini aliiomba mahakama itoe adhabu kali ili iwe funzo kwa
wanaume wote kwani kifo cha Naomi kimeonyesha kuambatana na mateso
makali na kufanya vijana na watu wengine kuwa na hofu kuingia katika
ndoa.
"Kuna jambo kubwa la kujifunza hapa kifo chake kilikuwa cha
kikatili , mateso, alikufa kifo cha kinyama hata jamii inajiuliza
anawezaje kufanya tukio kama hili,"alidai Mnzava akisaidiana na Wakili
wa Serikali Mkuu Yasinta Peter
Pia aliiomba mahakama ikabidhi
kielelezo namba PW8 ambacho ni mabaki wa mwili wa Naomi kwa familia yake
ili aweze kupewa heshima ya mwisho ya kidini ambayo hakupewa baada ya
kifo chake.
Jaji Mwanga alisema hilo ni kosa la mauaji mikono
yake imefungwa kiapo chake cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, kwa sheria za Tanzania adhabu ni moja tu kunyongwa hadi kufa.
"Nina
muhukumu Khamis Luwonga maarufu kwa jina la Meshack adhabu ya kunyongwa
hadi kufa, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mke wake Naomi
Marijani,"alisema Jaji Mwanga
Katika kesi hiyo ya mauaji namba
nne ya mwaka 2019, Mshtakiwa Luwongo ambaye ni Mkazi wa Kigamboni, Dar
es Salaam anadaiwa Mei 15, 2019 akiwa Gezaulole eneo la Kigamboni
alimuua Naomi Marijani.
Nje ya Mahakama
Baba mdogo wa
Marehemu, Robert Marijani alisema wameridhika na hukumu ilitolewa
maelezo aliyoyasema polisi ndiyo ndiyo hayo hayo
Mtoto wake
alikuwa mpambanaji, mjasiliamali mchakalikaji, laknii mume wake
(Meshack) alikuwa anataka awe tu mama wa nyumbani hakutaka
ajishughulishe
Alisema walipomuwezesha mtoto wao kufanya biashara
ndipo ikawa kero kwa mume wake kabla ya kifo hicho aliwahi kusuluhisha
ugomvi baina yao lakini huwezi kujua akili ya mtu.
Aidha,
wanatarajia kumzika Naomi upya, kwa kuchukua mabaki ya mwili ya mwili
wake katika kesi hii hakuna mwili wa marehemu kwa sababu yeye alienda
kuzika shambani wao wanachukua kwenda kumzika rasmi.
"Hatuwezi kumrudishia kwa sababu yeye aliamua kupandia migomba na wao wanataka kuzika rasmi,"alisema
Hata
baadhi ya ndugu, walisema kwa sasa watapumzika kidogo kwa sababu
walikuwa wakilia kila siku wakiiomba haki ipatikane ili wampumzishe
Naomi katika nyumba yake ya milele kwa kuzika mabaki yake.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...