Walipakodi mkoani Tabora wameahidi kuendelea kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kulipa Kodi kwa hiari na kuwafichua Wafanyabiashara wanaokwepa Kodi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano baina yao na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Juma Mwenda Wafanyabiashara hao wamesema wanajivunia kulipa Kodi kutokana na maendeleo makubwa yanayofanywa na serikali.

Alex Mlifwe, Isihaka Yange na Shaban Muhinda ni miongoni mwa Wafanyabiashara waliozungumza kwenye mkutano huo na kuiomba TRA kuwafikia Walipakodi wengi zaidi hasa waliopo katika maeneo ya vijijini.

Wamesema wapo watu wengi wanaofanya biashara bila kulipa Kodi Hali inayowaumiza wachache wanaolipa Kodi maana masoko wanayotumia ni ya aina moja na kushari wote wafikiwe.

Akizungumza na Wafanyabiashara hao pamoja na kujibu baadhi ya hoja za Wafanyabiashara Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda amewashukuru Walipakodi mkoani Tabora kwa kuendelea kuiunga mkono TRA kwa kulipa Kodi kwa hiari.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema kama ilivyo katika maeneo mengine amekutana na Wafanyabiashara hao kwa lengo la kuwashukuru na kusikiliza changamoto zao pia kuzipatia ufumbuzi ili kuweka mazingira rafiki katika ukusanyaji wa Kodi.

Amesema Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan alimuagiza wakati akimuapisha kuwa asimamie ukusanyaji wa Kodi bila kutumia nguvu na ndicho anachokisimamia hali ambayo imeongeza makusanyo ya Kodi na kufanya TRA ivuke malengo ya makusanyo kwa kipindi cha miezi 7 mfululizo.

Kuhusu watu wanaokwepa Kodi amewaomba Wafanyabiashara hao kushirikiana na TRA kuwafichua ili idadi ya walipakodi nchini iongezeke hali inayoweza kupunguza viwango vya Kodi.

Kuhusu suala la Elimu kwa Mlipakodi Kamishna Mkuu Mwenda amesema TRA inaendelea kutoa elimu ili kuwezesha walipakodi kutambua wajibu wao na kujua walipe kiasi gani, walipe muda gani na kwa namna gani.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...