MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amemjulia hali Mjumbe wa Halmashauri Kuu yaTaifa (NEC), Ndugu Christopher Gachuma ambaye amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Bugando jijini Mwanza.


Ndugu Gachuma amelazwa hospitalini hapo baada ya kupata ajali ya gari jana katika Kijiji cha Gesarya, Kata ya Lung'abure, wilayani Serengeti Mkoa wa Mara alipokuwa akielekea katika Ziara ya Makamu Mwenyekiti Wasira.

Majeruhi mwengine katika ajali hiyo ni Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Ndugu Kemilembe Ruta pamoja na dereva wa gari hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya hospitali hiyo, majeruhi wote wa ajali hiyo wanaendelea vizuri.

Ndg Wasira amewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ambapo kesho atahutubia mkutano mkubwa utakaofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini humo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...