 
 
Ndola, Zambia: 
 Mwenyekiti wa Bodi ya ya Wakurugenzi ya EWURA, Prof. Mark Mwandosya leo
 23 Machi 2025, ameongoza wajumbe wa Bodi hiyo na Menejimenti kwenye 
ziara ya kutembelea Bomba la Mafuta la TAZAMA linaloanzia Dar es Salaam,
 Tanzania hadi Ndola, Zambia. Ziara hiyo ilianza Machi 21, 2025. 
Mwenyekiti
 wa Kamati ya Nishati ya Bodi hiyo, Mha. Ngosi Mwihava alisema lengo la 
ziara hiyo ni kutizama utekelezaji wa masuala ya kiuchumi, kimiundombinu
 na uendeshaji wa bomba la TAZAMA. 
“Moja ya jukumu la EWURA 
katika sekta ya petroli ni kudhibiti miundombinu ya usafirishaji wa 
mafuta na gesi asilia, hivyo ziara hii ni mahsusi kwa ajili ya 
kutembelea miundombinu ya bomba, kuona changamoto zilizopo na kuangalia 
namna tunavyoweza kusaidia utatuzi wa changamoto hizo ili kuendelea 
kuboresha huduma za usafirishaji wa mafuta kupitia bomba hili” alisema. 
Mha.
 Mwihava aliongeza kuwa, ziara hiyo ni fursa kwa Bodi ya EWURA na ya 
Udhibiti wa Nishati Zambia (ERB) kubadilishana uzoefu katika maeneo 
mbalimbali ikiwemo ya upangaji wa bei, mikakati ya uhifadhi wa mafuta ya
 akiba na kujengea wataalamu uwezo. 
Ujumbe huo pia, umetembelea 
kituo cha Chilolwa cha kuangalia usalama wa bomba la mafuta, kituo cha 
kusukuma mafuta kilichopo Chinsali na ghala la kuhifadhia mafuta 
lililopo Mpika. 
Maeneo mengine yaliyotembelewa ni kituo cha 
Kilonje cha kusukuma mafuta, kituo cha Mulilima cha kutuma na kupokelea 
kifaa cha kufanya usafi wa bomba, na kituo cha kupokelea mafuta cha 
Bwana Mkubwa ambacho kiko Ndola. 
Ujumbe huo pia utakutana na 
uongozi la Bomba la TAZAMA, Bodi ya Wakurugenzi ya Taasisi ya Udhibiti 
wa Nishati Zambia (ERB) pamoja na Baraza la Udhibiti wa Huduma za Maji 
na Usafi wa Mazingira Zambia (NWASCO) ili kujadili masuala mbalimbali ya
 ushirikiano wa kisekta.  
  
  
  
  
 
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


 
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...