Na Mwandishi Wetu

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara John Mongella ameshiriki Ibada ya Shukrani ya kumbukizi ya miaka minne ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Magufuli, aliyefariki dunia Machi 17 mwaka 2021.

Akiwasilisha salamu za CCM kwa niaba ya Katibu Mkuu, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo Machi 17,2025 Mongella amesema kuwa Chama kitaendelea kumuenzi Hayati Dkt. Magufuli kwa kazi kubwa aliyoifanya katika ujenzi wa Taifa na ustawi wa Chama.

Wakati huo huo katika harambee ya kumalizia ujenzi wa Kanisa la Katoliki Chato, Geita, Mongella ametangaza kuwa CCM itachangia Shilingi milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo, ambalo ni miongoni mwa miradi iliyoasisiwa na Hayati Magufuli.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...