Madaktari bingwa wa mpango wa Mama Samia kutoka mikoa mbalimbali wametoa mafunzo ya kuboresha utoaji huduma kwa mama na watoto wachanga kwa watumishi wa afya wa Hospitali ya Wilaya ya Singida na vituo vya afya jirani.

Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo watoa huduma, hasa katika sekta ya afya ya mama na mtoto, ili kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga. Mafunzo hayo ya siku tatu yalifanyika kuanzia tarehe 17 hadi 19 Machi, 2025, katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya ya Singida.

Watumishi wa afya walioshiriki wameeleza shukrani zao kwa madaktari hao kwa ujuzi waliopata na wameahidi kutumia maarifa hayo kuboresha utoaji huduma na kuongeza weledi katika kazi zao za kila siku.

Mpango huu ni moja ya juhudi za serikali za kuimarisha huduma za afya nchini na kuhakikisha mama na mtoto wanapata huduma bora na salama.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...