Wadau mbalimbali wa maendeleo Nchini Tanzania wamekutana jijini dar es salaam kama sehemu ya kujadili maswala mbalimbali yanayohusu utunzaji wa viumbe hai kupitia Mradi wa Biodiversity finance initiative uliozinduliwa jijini Dar es salaam na naibu katibu Mkuu ofisi ya makamu wa Rais Mh. HASSAN MOHAMED HASSAN

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, ABDALLAH HASSAN MITAWI amesema mabadiliko ya tabianchi yana mchango mkubwa katika kuathiri viumbe hai na Mazingira nchini Tanzania ameyasema hayo katika uzinduzi wa Mradi wa Biodiversity finance initiative ululiozinduliwa kwa mara ya kwanza Tanzania Bara

 

 

Kwa upande mwingine mchambuzi wa programu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) FERISTER IGNATUS amepongeza dhamira ya Tanzania Bara katika kuunga mkono mpango wa kudhithibi uwepo wa viumbe hai na Mazingira salama kwa jamii

 

 

HASSAN MOHAMED HASSAN ambaye ni mratibu wa BIOFIN Zanzibar ameeleza sababu zinazopelekea Zanzibar kupata mafanikio katika mipango ya kutunza Viumbe hai kupitia Mradi wa Biodiversity finance initiative ambapo sera wezeshi na usimamizi mzuri zinatajwa kuwa sababu kuu za kufanikiwa kwa Mradi huu

 

 

Mradi wa Biodiversity finance initiative unatajwa kuleta mageuzi Tanzania Bara mara baada ya kuzinduliwa kwa mara ya kwanza huku wadau mbalimbali wa maendeleo wakiunga mkono sera ya utunzaji viumbe hai













Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...