Na Mwandishi wetu

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, ameitunuku Benki ya NMB cheti cha shukrani kwa mchango wake katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Kahimba, wilayani Buhigwe, mkoani Kigoma.

Akipokea cheti hicho kwa niaba ya benki, Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Restus Assenga, alieleza kuwa NMB itaendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu, hasa kwa wasichana, kama sehemu ya dhamira yake ya kuleta maendeleo endelevu katika jamii.

Sherehe hiyo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto, Mhe. Thobias Andengenye, Meneja Mahusiano ya Benki na Serikali wa NMB Kanda ya Magharibi, Suma Mwainunu, Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Kanali Michael Ngayalina, na Meneja wa NMB Tawi la Buhigwe, Pendo Waziri.

Mchango wa NMB katika mradi huu ni sehemu ya azma ya benki hiyo kusaidia maendeleo ya sekta ya elimu nchini kupitia uwekezaji wa rasilimali katika miundombinu ya shule ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...