Na Mwandishi Wetu,Kagera

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amewasili mkoani Kagera kuanza ya kikazi ya siku nne.

Wasira amepokelewa leo Machi 22, 2025 katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba akiwa ameongozana na viongozi mbalimbali wakiwemo baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM.

Ziara hiyo ina lengo la kukagua uhai wa Chama, utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025, kusikiliza changamoto za wananchi pamoja na kuhutubia mikutano ya hadhara ambapo katika siku ya kwanza atahutubia mkutano mkubwa Kata ya Kemondo, Wilaya Bukoba.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...