WAKAZI wa nne Same mkoani Kilimanjaro  wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi wakikabiliwa na kesi ya Uhujumu Uchumi yenye mashtaka ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya Mirungi ya jumla ya kilogramu 518.57.

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo  leo Machi 28,2025 na wakili wa serikali Julieth Komba imewaja washtakiwa hao kuwa ni Nimkaza Mbwambo, Prosper Lema, Nterindwa Mngalle maarufu kama mama Dangote na Stephano Mrutu.

Washtakiwa wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ally Mkama ambapo kila mmoja amesomewa kosa lake.

Mshtakiwa Nimkaza anadaiwa kukutwa akisafirisha dawa za kulevya aina ya Mirungi zenye uzito wa kiligramj 138.58, Machi 21, 2025 huko katika kijiji cha Rikweni Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Mshtakiwa  Prosper Lema yeye anadaiwa kuwa siku na mahali hapo alikutwa akisafirisha kilogramu 113.29 za dawa za kulevya aina ya Mirungi

Mshtakiwa Nterindwa Mngalle anadaiwa Machi 21,2025 huko katika kijiji cha Rikweni Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro alikutwa akisafirisha dawa za kulevya aina ya Mirungi zenye uzito wa kilogramu160.25.

Naye mshtakiwa Stephanie Mrutu amefikishwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu  Mkama kujibu shtaka la kukutwa na kilogramu 106.45 za dawa za kulevya aina ya Mirungi.

Wakati huo huo, washtakiwa wawili, Dorisiana Mchome na Aisha Mbaga wa Same, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Same wakikabiliwa na shtaka la kusafirisha dawa za kulevya aina ya Mirungi zenye uzito wa kilogramu 54.15

Washtakiwa wamesomewa kila mmoja shtaka lake mbele ya Hakimu Mkazi Hellen Hozza ambapo wanadaiwa kutenda kosa hilo Machi 21, Huko Rikweni kata ya Tae wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Wakili wa serikali Michael Matowo amedai siku na mahali hapo mshtakiwa Dorisiana alikutwa akisafirisha kilogramu 17 za dawa za kulevya aina ya Mirungi huku mshtakiwa Aisha Mbaga akidaiwa kusafirisha dawa za kulevya aina ya Mirungi yenye uzito wa kilogramu 37.15

Hata hivyo washtakiwa waliofikishwa katika mahakama ya Moshi  wamerudishwa rumande hadi Aprili 11 mwaka huu kesi hiyo Itakapokuja kwa ajili ya kutajwa wakati washtakiwa walifikishwa mahakama ya Same wamerudishwa rumande hadi Aprili 10,mwaka huu

Hivi karibuni Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) ilifanya operesheni maalum wilayani Same, mkoani Kilimanjaro, ambapo ekari 285.5 za mashamba ya mirungi ziliteketezwa. Katika operesheni hiyo, mfanyabiashara Interindwa Kirumbi, maarufu kama Mama Dangote, alikamatwa pamoja na wenzake kwa tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya mirungi. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa katika biashara hiyo kwa zaidi ya miaka 30, akisimamia mitandao ya usambazaji wa mirungi nchini.

Serikali, kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya na Wizara ya Kilimo na Mifugo, imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya mirungi na kuwawezesha kujikita katika kilimo cha mazao mbadala na ufugaji. Miradi kama ufugaji wa nguruwe na miche ya kahawa imeanzishwa ili kuwasaidia wakulima kuachana na kilimo cha mirungi. Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, amesisitiza kuwa operesheni dhidi ya biashara ya mirungi itaendelea ili kuhakikisha inatokomezwa kabisa nchini.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...