NA. MWANDISHI WETU BERLIN, UJERUMANI


Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, na Uratibu, Mhe. Ummy Nderiananga, amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bi. Gérardine Mukeshimana, katika kikao cha pembezoni mwa Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Watu Wenye Ulemavu uliofanyika tarehe 2–3 Aprili, 2025 mjini Berlin, Ujerumani.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Ummy amesisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania kuendeleza ushirikiano na IFAD katika kuimarisha miradi ya kilimo inayolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa maendeleo jumuishi.

Viongozi hao wamejadili  umuhimu wa kuweka mikakati madhubuti ya maendeleo jumuishi ili kuhakikisha  programu za kilimo zinakuwa shirikishi, zenye usawa, na zenye manufaa kwa jamii nzima.

Kupitia IFAD, Tanzania inaendelea kutekeleza Mradi wa Maendeleo ya Kilimo na Uvuvi (AFDP) na Mradi wa Mageuzi ya Sekta ya Maziwa kwa Njia Endelevu ya Hali ya Hewa (C-SDTP), miradi inayochangia ustawi wa wananchi na kujenga mazingira jumuishi kwa watu wenye ulemavu katika sekta ya kilimo na mifugo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...