Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la taasisi za umma katika Maonyesho ya Kwanza ya Mfuko wa Utamaduni yaliyofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 30 Aprili, 2025 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
TEA ilikuwa miongoni mwa taasisi zaidi ya 30 zilizoshiriki katika maonyesho hayo yaliyoandaliwa na Mfuko wa Utamaduni, kwa lengo la kuhamasisha na kuendeleza shughuli za kitamaduni nchini.
Vigezo vilivyotumika katika kutoa tuzo hizo ni pamoja na muonekano wa banda, utoaji wa huduma kwa wageni waliotembelea banda, pamoja na muda wa kufungua na kufunga huduma.
Tuzo hizo zilitolewa na Mgeni Rasmi, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Prof. Paramaganda Kabudi, ambaye alipongeza taasisi zote zilizoshiriki kwa mchango wao katika kufanikisha maonyesho hayo.







TEA ilikuwa miongoni mwa taasisi zaidi ya 30 zilizoshiriki katika maonyesho hayo yaliyoandaliwa na Mfuko wa Utamaduni, kwa lengo la kuhamasisha na kuendeleza shughuli za kitamaduni nchini.
Vigezo vilivyotumika katika kutoa tuzo hizo ni pamoja na muonekano wa banda, utoaji wa huduma kwa wageni waliotembelea banda, pamoja na muda wa kufungua na kufunga huduma.
Tuzo hizo zilitolewa na Mgeni Rasmi, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Prof. Paramaganda Kabudi, ambaye alipongeza taasisi zote zilizoshiriki kwa mchango wao katika kufanikisha maonyesho hayo.








Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...