Na Mwandishi wetu


MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Watumishi Housing Investment (WHI), AbdulRazak Badru ametoa wito kwa watumishi wa Umma kuchangamkia fursa ya uwekezaji kupitia dirisha E-Wekeza linalotarajiwa kuzinduliwa na serikali kupitia mfumo wa watumishi portal hivi karibuni. 
Badru ameyasema hayo wakati akizungumza na wawekezaji na wajumbe wa bodi katika Mkutano Mkuu wa pili wa Mfuko wa Uwekezaji wa Faida 2025 ujulikanao kama Faida Fund.

 Badru Pia ameiomba Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhimiza na kuwakumbusha watumishi wa umma kushiriki katika kuwekeza kwa mwendelezo ili kujiwekea akiba kidogo kidogo Kwa manufaa yao ya Sasa na baadae.

 Kwa upande wake Mwakilishi wa kutoka Ofisi ya Rais-Utumishi Bi. Leila mavika Kwa niaba ya  katibu mkuu Utumishi wa Umma amesema wako tayari kushirikiana ili kuhakikisha mfumo inasomana na kurahisisha huduma kwa watumishi kuwekeza katika mifuko mbalimbali ikiwemo Faida Fund.
















 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...