Na Issa Mwadangala

Wasafirishaji wa abiria kwa kutumia pikipiki (Bodaboda) kijiwe cha Shingo feni kilichopo Kijiji cha Lumbila Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe wametakiwa kuepukana na vitendo vya kujihusisha na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi ikiwa ni pamoja na kufuata na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepukana na ajali ambazo zinaweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo ulemavu wakudumu.

Kauli hiyo imetolewa Mei 14, 2025 na Polisi kata ya Ruanda Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Happy Lumbe ambapo amewataka wasafirishaji hao kuacha tabia ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi pia wasisite kutoa taarifa za wenzao wenye tabia kama hizo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa haraka dhidi yao na iwe fundisho kwa jamii.

Kwa kuongezea na kumalizia Mkaguzi Lumbe amewataka wasafirishaji hao kuacha na kuepukana na tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwani ni kosa kisheria.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...