Katibu Mkuu Kiongozi Balozi, Dkt. Moses Kusiluka, akizungumza na maafisa wa Taasisi za Umma na Binafsi kwenye kikao cha mwezi kilichofanika jijini Dodoma Mei 2, 2025.


RAIS wa Taasisi ya Wakaguzi wa Ndani Tanzania, Dk. Zelia Njeza (kushoto) akikabidhi zawadi kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusiluka baada ya kufungua Mkutano wa Mwezi wa Ukaguzi wa Ndani uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma jana. Kulia ni Mkaguzi Mkuu wa ndani, Benjamin Magai.

RAIS wa Taasisi ya Wakaguzi wa Ndani Tanzania, Dk. Zelia Njeza (kushoto) akikabidhi zawadi kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusiluka baada ya kufungua Mkutano wa Mwezi wa Ukaguzi wa Ndani uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma jana. Kulia ni Mkaguzi Mkuu wa ndani, Benjamin Magai.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

KATIBU Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka ametoa wito kwa taasisis za Umma na Binafsi  kuendelea kushirikiana kwa karibu na kuwaamini wakaguzi wa ndani ili kusadia kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu kwa lengo la kusaidia kupunguza makosa yanayosababisha hati chafu na badala yake kuleta maendeleo chanya  katika taasisi na Taifa kwa Ujumla.

Balazi Dkt.KUSILUKA ameyasema hayo Jijini Dodoma kwenye kikao cha mwezi cha maaafisa ukaguzi wa ndani ambapo amesema ni muhimu kufanya kazi kwa kuzingatia welezdi na kufanya kazi kwa uwazi ili kufanikisha malengo ya taasisi na Taifa.

Kwa upande wake Rais wa Taasisi ya wakaguzi wa Ndani Tanzania (IIA) DKT. ZELIA NJEZA ameziomba  taasisi za Umma na Binafsi Nchini  kutoa ushirikiano kwa wakaguzi wa ndani ili wasaidie kuwapa Elimu juu uendeshaji wa  taasisi hizo ili zifanye kazi kwenye mlengo sahihi.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...