Katika kuunga mkono falsafa ya UTU NA MAENDELEO inayoasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Madaktari Wanawake wa Kiislam nchini wamezindua rasmi Mfuko wa Kusaidia Huduma za Afya kwa Watoto Wenye Uhitaji, unaojulikana kama Muslimah Medical Support Fund (MMSF).
Mfuko huu ni mwendelezo wa juhudi za kujitolea ambazo madaktari hao wamekuwa wakizifanya kwa muda katika utaratibu usio rasmi, ambapo wamekuwa wakisaidia watoto kutoka familia zisizo na uwezo kupata matibabu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mwenyekiti wa MMSF Dkt. Asha Omari Mahita alisema kuwa wazo hilo lilianza kupitia mawasiliano ya kawaida katika kundi la WhatsApp, baada ya madaktari kuguswa na mateso ya watoto wanaokosa huduma muhimu za afya kutokana na ukosefu wa rasilimali.
“Kwa mujibu wa maadili ya Uislamu, huduma ya afya ni haki ya msingi kwa kila binadamu. Tumeona ni wajibu wetu kusaidia kundi hili linaloathirika zaidi, kwa kuanzia na watoto, mpaka Sasa tumekwisha wakatia bima za Afya watoto 500 na malipo ya moja kwa moja hospitalini bila kujali ni dini gani” alisisitiza Dkt. Mahita.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mstaafu, Prof. Mussa J. Assad, aliwapongeza Madaktari hawa Wanawake kwa moyo wao wa kujitolea na kuonyesha mfano bora wa uwajibikaji wa kijamii. Alisisitiza umuhimu wa kutumia uzoefu wa madaktari waliostaafu ili kupanua huduma kwa walengwa zaidi.
“Mfuko huu unaonyesha dira sahihi ya mshikamano wa kitaifa na matendo yenye kugusa maisha ya wengi. Ninafurahishwa na muundo wa MMSF ambao ni himilivu na unaolenga kupanua wigo wa huduma kwa kushirikiana na wadau mbalimbali,” alisema Prof. Assad.
Waanzilishi wa MMSF wamesema wanatarajia kushirikiana na hospitali, taasisi, watubinafsi na wahisani mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto kutoka familia zisizo na uwezo wanapata huduma za kitabibu zenye ubora bila vikwazo vya kifedha.
Katika malengo mengine Karibu wa MMSF Dr Khadija Ibrahim alisema malengo ya mbeleni ni pamoja na kusaidia ada kwa waschana waliokwana wanotaka kuwa madaktari na pia kuweka Kambi za kitabibu (Medical camp) vijijini.
Mfuko huu ni mwendelezo wa juhudi za kujitolea ambazo madaktari hao wamekuwa wakizifanya kwa muda katika utaratibu usio rasmi, ambapo wamekuwa wakisaidia watoto kutoka familia zisizo na uwezo kupata matibabu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mwenyekiti wa MMSF Dkt. Asha Omari Mahita alisema kuwa wazo hilo lilianza kupitia mawasiliano ya kawaida katika kundi la WhatsApp, baada ya madaktari kuguswa na mateso ya watoto wanaokosa huduma muhimu za afya kutokana na ukosefu wa rasilimali.
“Kwa mujibu wa maadili ya Uislamu, huduma ya afya ni haki ya msingi kwa kila binadamu. Tumeona ni wajibu wetu kusaidia kundi hili linaloathirika zaidi, kwa kuanzia na watoto, mpaka Sasa tumekwisha wakatia bima za Afya watoto 500 na malipo ya moja kwa moja hospitalini bila kujali ni dini gani” alisisitiza Dkt. Mahita.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mstaafu, Prof. Mussa J. Assad, aliwapongeza Madaktari hawa Wanawake kwa moyo wao wa kujitolea na kuonyesha mfano bora wa uwajibikaji wa kijamii. Alisisitiza umuhimu wa kutumia uzoefu wa madaktari waliostaafu ili kupanua huduma kwa walengwa zaidi.
“Mfuko huu unaonyesha dira sahihi ya mshikamano wa kitaifa na matendo yenye kugusa maisha ya wengi. Ninafurahishwa na muundo wa MMSF ambao ni himilivu na unaolenga kupanua wigo wa huduma kwa kushirikiana na wadau mbalimbali,” alisema Prof. Assad.
Waanzilishi wa MMSF wamesema wanatarajia kushirikiana na hospitali, taasisi, watubinafsi na wahisani mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto kutoka familia zisizo na uwezo wanapata huduma za kitabibu zenye ubora bila vikwazo vya kifedha.
Katika malengo mengine Karibu wa MMSF Dr Khadija Ibrahim alisema malengo ya mbeleni ni pamoja na kusaidia ada kwa waschana waliokwana wanotaka kuwa madaktari na pia kuweka Kambi za kitabibu (Medical camp) vijijini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...