
Na John Mapepele
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa leo ameweka jiwe la msingi kwenye jengo la utawala la jiji la Arusha na kushuhudia utiaji wa saini mikataba ya mradi wa Stendi Kuu ya Mkoa wa Arusha, Soko la Mrombo na Bustani ya Mapumziko ya Themi vyote vikiwa thamani ya takriban shilingi bilioni 40.
Akikagua ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya jiji la Arusha lenye sakafu tisa ambalo litakapokamilika litagharimu bilioni 9.8 amemtaka mkandarasi kukamilisha ujenzi kwa wakati ili kuondokana na adha ya sasa ya watumishi kufanyia kazi kutokea kwenye ofisi zilizo katika maeneo tofauti hali inayochelewesha utoaji wa huduma kwa wananchi.
"Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuridhia kutoa fedha za ujenzi wa jengo hili kwa kuwa baada ya kukamilika litakuwa mkombozi kwa watumishi" . Amefafanua Mhe. Mchengerwa

Aidha ameuelekeza uongozi wa Mkoa na Jiji la Arusha kuhakikisha jengo hilo linakamilika mara moja na endapo kutakuwa na mkwamo wowote wachukue hatua.
Amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda kwa kukwamua mgogoro wa kushindwa kukamilika kwa jengo hilo kwa zaidi ya miaka 5 kutokana na masuala ya kisiasa.
Mradi huo umefikia asilimia 62 na unafanywa na mkandarasi mzawa M/S Tribe Construction Ltd na unatarajiwa kukamilika Julai mwaka huu.
Akihutubia wananchi baada ya kushuhudia utiaji wa saini mikataba ya mradi wa ujenzi wa Stendi Kuu ya Mkoa wa Arusha na Soko la Mrombo na Bustani ya Mapumziko ya Themi, Mhe. Mchengerwa amewataka viongozi kufanya maaamuzi magumu katika kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye.

Miradi hiyo ambayo inatarajia kugharimu bilioni 30.6 itakapokamilika ametaka iwe inaweza kujiendesha yenyewe na kutoa faida.
Pia amesisitiza kuilinda, na kufanya usafi ili iwezekudumu kwa muda mrefu pindi itakapokamilika.
"Jukumu letu ni kuitunza miundombinu hii itakayojengwa kwa gharama kubwa ili iweze kudumu kwa muda uliotarajiwa. Aidha, naelekeza Halmashauri zenye Miradi yenye kujiendesha kama Masoko na Stendi zihakikishe miradi hiyo inajiendesha na kuzalisha mapato kwenye Halmashauri husika." Amesisitiza Mhe. Waziri
Pia amesisitiza kuilinda, na kufanya usafi ili iwezekudumu kwa muda mrefu pindi itakapokamilika.
"Jukumu letu ni kuitunza miundombinu hii itakayojengwa kwa gharama kubwa ili iweze kudumu kwa muda uliotarajiwa. Aidha, naelekeza Halmashauri zenye Miradi yenye kujiendesha kama Masoko na Stendi zihakikishe miradi hiyo inajiendesha na kuzalisha mapato kwenye Halmashauri husika." Amesisitiza Mhe. Waziri

Amemtaka mkandarasi kufanya kazi kwa haraka na kukamillisha kulingana na mkataba na mpango kazi uliokubalika ili wananchi wa Jiji la Arusha waanze kunufaika na miundombinu hiyo ambayo Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza katika jijini Arusha.
Aidha, amemtaka mkandarasi mshauri kuhakikisha mikataba hiyo inasimamiwa kikamilifu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi na TARURA ili ikamilike ndani ya muda uliopangwa, lakini pia katika ubora uliokubalika ili thamani ya fedha ionekane.
Pia amewaagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri wasimamie kikamilifu utekelezaji wa miradi hiyo kwa kutumia rasilimali watu na vifaa vilivyopo kwenye Halmashauri husika.
Waziri Mchengerwa amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali zenye lengo la kuboresha maisha ya Wananchi. Mojawapo ya hatua zinazochukuliwa ni kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, Masoko, pamoja utunzaji wa Mazingira katika maeneo ya mijini chini ya Mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji ya Tanzania kwa kuhusisha Ushindani ambao kitaalam unajulikana kama Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness (TACTIC) Project.
"Ndugu Wananchi, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi thabiti wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatekeleza kwa vitendo falsafa ya maendeleo jumuishi. Miradi tunayoizindua leo kupitia Mradi wa TACTIC siyo miundombinu pekee bali ni daraja kati ya leo na kesho bora zaidi kwa wananchi wetu." Amesisitiza
Amesema miradi hiyo inatekelezwa kupitia Mkopo wa Benki ya Dunia utakaogharimu kiasi cha Dola za Kimarekami Milioni 410 na inatekelezwa katika miji 45 mbalimbali nchini. Lengo kuu la mradi wa TACTIC ni kuboresha usimamizi wa ukuaji wa Miji pamoja na kuziwezesha Halmashauri za Miji na Majiji kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha, amemtaka mkandarasi mshauri kuhakikisha mikataba hiyo inasimamiwa kikamilifu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi na TARURA ili ikamilike ndani ya muda uliopangwa, lakini pia katika ubora uliokubalika ili thamani ya fedha ionekane.
Pia amewaagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri wasimamie kikamilifu utekelezaji wa miradi hiyo kwa kutumia rasilimali watu na vifaa vilivyopo kwenye Halmashauri husika.

Waziri Mchengerwa amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali zenye lengo la kuboresha maisha ya Wananchi. Mojawapo ya hatua zinazochukuliwa ni kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, Masoko, pamoja utunzaji wa Mazingira katika maeneo ya mijini chini ya Mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji ya Tanzania kwa kuhusisha Ushindani ambao kitaalam unajulikana kama Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness (TACTIC) Project.
"Ndugu Wananchi, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi thabiti wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatekeleza kwa vitendo falsafa ya maendeleo jumuishi. Miradi tunayoizindua leo kupitia Mradi wa TACTIC siyo miundombinu pekee bali ni daraja kati ya leo na kesho bora zaidi kwa wananchi wetu." Amesisitiza
Amesema miradi hiyo inatekelezwa kupitia Mkopo wa Benki ya Dunia utakaogharimu kiasi cha Dola za Kimarekami Milioni 410 na inatekelezwa katika miji 45 mbalimbali nchini. Lengo kuu la mradi wa TACTIC ni kuboresha usimamizi wa ukuaji wa Miji pamoja na kuziwezesha Halmashauri za Miji na Majiji kutoa huduma bora kwa wananchi.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...