Na. Josephine Majura, WF, Dodoma

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amesema kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ina mpango wa kuanza ujenzi wa Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara, katika mwaka 2026/27.

Aliyasema hayo bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Zacharia Paulo Issaay, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya hiyo.

Alifafanua kuwa katika kipindi ambacho hakuna Ofisi ya TRA, shughuli za ukusanyaji wa mapato ya Serikali zinafanyika kwenye jengo la iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akijibu swali la  Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Zacharia Paulo Issaay, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu, jijini Dodoma.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Wizara ya Fedha)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...