Serikali ya awamu ya sita ikishikirikiana na sekta binafsi imedhamiria kuja na mpango wa kuanzisha vituo vya ukodishaji wa mitambo ya uchimbaji madini ambapo mitambo hii itaenda kuwa mwanga kwa wakulima pia.

Hayo yamesemwa na waziri wa madini Antony Mavunde wakati wa kilele cha kongamano la wachimbaji madini lililofanyika katika mamlaka ya mji mdogo Katoro mkoani Geita.

Mavunde alisema kuwa mitambo hii ya kukodi itaenda kuwa msaada mkubwa katika shughuli za uchimbaji hususani wachimbaji wadogo ambao walilazimika kununua mitambo mipya kwa gharama kubwa.

" Ukienda kwa wakulima, sio kila mkulima ana trekta la kulimia kwasababu ni ghalama kubwa kumililiki trakta wqchimbaji wadogo pia mmekuwa mkihangaika kupata mitambo sio kila mchimbaji mdogo anaweza kuwa na mitambo hii ndio maana serikali imekuja na mpango huu" alisema Mavunde

Aliongeza kuwa serikali imeshazungumza na sekta binafsi na kwamba wapo tayari kuanzisha kituo katika mkoa wa Geita ili kurahisisha kazi wachimbaji wadogo.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...