SERIKALI ya Tanzania imeendelea kupata pongezi kutoka kwa wawekezaji wa kigeni kwa jitihada zake za kuboresha mazingira ya biashara, ikiwemo kurahisisha taratibu za usajili wa kampuni na kuwapa wawekezaji fursa ya kuanza shughuli haraka bila vikwazo vikubwa vya kiutendaji.
Ameeleza kwamba Spidd Africa, kampuni yenye makao makuu nchini Uganda, inalenga kuleta mageuzi ya kidijitali katika sekta ya biashara barani Afrika kupitia suluhisho bunifu, hususani kwa wajasiriamali wadogo, biashara za kati, na mashirika makubwa.
Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Spidd Afrika kutoka Uganda,
Angela Semwogerere, amebainisha kwamba moja ya malengo makuu ya kampuni hiyo ni
kutoa elimu na mafunzo kuhusu usalama wa kimtandao kwa taasisi mbalimbali, ili
kuongeza uelewa na ulinzi wa taarifa katika ulimwengu wa kidijitali.
Kufunguliwa kwa tawi la Spidd Africa nchini kunatarajiwa kuchochea mabadiliko chanya katika sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano, pamoja na kukuza ajira na ubunifu kwa vijana wa Kitanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...