Na. Vero Ignatus,Siha Kilimanjaro


Uzinduzi wa West Kili Forest Tour Challenge 2025 umefanyika rasmi mei 23,2025 lengo kuu likuwa ni kuinua Utalii Endelevu na Uchumi wa Kijani,kutangaza utalii wa ikolojia,vivutio vilivyopo na kutoa elimu ya uhifadhi kwa vitendo pamoja na kuona fursa zanuweiezaji ndani ya hifadhi ya shamba la Miti West Kilimanjaro.

Akizungumza wakati akitoa salamu kwa mgeni rasmi,wadau wa mazingira, wawakilishi wa sekta ya utalii, wananchi na waandishi wa habari, Mhifadhi mkuu Hifadhi ya Msitu West Kilimanjaro PCO. Robert Faida, alisema kuwa hiyo ni fursa ya pekee kuwakutanisha wadau wa utalii na kutengeneza mtandao wa biashara, kukuza utalii na uchumi

Aidha PCO Faida amesema tukio la mwaka huu linatarajiwa kuwa na washiriki zaidi ya 2,000 na kuweka West Kilimanjaro kwenye ramani ya Kimataifa ya utalii wa Mazingira hivyo TFS iliona ni vyema kutumia vivutio hivyo vya utalii kutangaza utalii, ambapo amewakaribisha Sekta binafsi kushirikiana na TFS katika kuendeleza eneo hilo.

"Hapa washiriki wanapata elimu kwa vitendo na kuona umuhimu wa uhifadhi kwani nieneo la kimkakati na shindani hivyo itatusaidia kutangaza fursa za uwekezaji zinazoweza kufanyika ndani ya hifadhi, kwa uwepo kwa mlima Kilimanjaro na root ya Lemotsho, wageni wengi wanaigia, vile vile washiriki wetu wa mbio hizi wanakutana na kutengeneza mtandao wa kibiashara "Alisema Faida.

Akizungumza Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dkt. Christopher Timbuka,amesema msimu huo wa tano wa West Kili Forest Tour Challenge 2025, ni tukio

kubwa linalotarajiwa kufanyika tarehe 21 hadi 22 Juni 2025 katika misitu ya West Kilimanjaro, Wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro.

Dkt. Timbuka alieleza kuwa lengo la tukio hilo ni kukuza utalii endelevu,uhifadhi elimu, uwekezaji na kuhamasisha uhifadhi wa mazingira kuwakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali kwa lengo la kushirikiana katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi, amewahimiza wananchi kinjtokeza kwa wingi kushiriki kwani kuna manufaa ya moja kwa moja kwa jamii, siyo tu katika nyanja ya uchumi,

"Tukio hili tunatarajia kuwa na washiriki kutoka ndani na nje ya nchi kwa shughuli mbalimbali zitakazofanyika ndani ya hifadhi, zikiwemo matembezi na mbio za umbali wa kilomita 21,10 na 5 kwa ajili ya kujionea mandhari ya kipekee ya misitu ya West Kilimanjaro; mbio za baiskeli na moto-cross; maonyesho ya mavazi ya asili, michezo ya watoto, pamoja na ngoma na sanaa za jadi. Alisema Dkt Timbuka.

Amesema usajili wa washiriki wa mwaka huu umerahisishwa kwa njia mbili kuu: moja ni kupitia mtandao kwa kutembelea tovuti rasmi ya www.westkili.co.tz au tickets.westkili.co.tz, na nyingine ni kwa kufanya malipo ya moja kwa moja kwa simu kupitia namba ya Tigo 7878284 kwa jina West Kili Run and Bike au M-Pesa 5362338 kwa jina Pedal Tz.

Azungumza kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Profesa Dos Santos Silayo,Mhifadhi Mwandamizi, Tulizo Kilaga alisema kuwa West Kili Challenge inaakisi mkakati wa TFS wa kutumia misitu kama kichocheo cha uchumi, na kuongeza kuwa tukio hili linaendana na dira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kukuza uchumi wa kijani na kuhakikisha misitu inanufaisha kizazi cha sasa na kijacho.

"Mhe. Mkuu wa wilaya Prof anatambua kazi kubwa inayofanywa katika wilaya yako katika promotion ya utalii ameniambia nikwambie kwa mwaka huu TFS imevunja rekodi katika mapato ya utalii ambapo tumefika zaidi ya Bil 2 na huku West Kilimanjaro ni kituo kinachoongoza kwa mapato ya TFS. Alisema Kilaga.

"Tunapotangaza ‘Explore Life in Nature,’ tunawaalika Watanzania kuiona TFS ni fursa pia zaidi ya kuni,mkaa, mbao,tumetoka huko utalii wa mazingira umeshika chati na unsingiza maps to kwa kiasi kikubwa,alisema Kilaga.
Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dkt. Christopher Timbuka,akizindua rasmi. msimu wa tano wa West Kili Forest Tour Challenge 2025, ndani ya Hifadhi shamba la Miti West Kilimanjaro





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...