Na Kassim Nyaki, Dodoma
Wabunge wameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa jitihada kubwa za kutangaza vivutio vya utalii, ambazo zimesaidia kuongeza idadi ya watalii wa kimataifa kutoka 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia 2,141,895 mwaka 2024, huku watalii wa ndani wakiongezeka kutoka 788,933 hadi 3,218,352 katika kipindi hicho.
Kwa upande wa maduhuli ya Serikali yametajwa kuongezeka kutoka Shilingi bilioni 397.42 Mwaka 2020/2021 hadi Shilingi bilioni 901.08 Mwaka 2023/2024. Aidha mwaka wa Fedha 2024/2025 kuanzia Julai 2024, hadi kufikia Aprili 2025, Wizara imekusanya jumla ya Shilingi bilioni 912.90 sawa na asilimia 94.2 ya lengo la makusanyo, kiwango ambacho ni kikubwa kuliko wakati wowote kuwahi kupatikana katika historia ya sekta hii
Pongezi hizo zimetolewa wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii 2025/26 iliyowasilishwa na Waziri Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana, ambaye ameomba Bunge liidhinishe Sh. bilioni 359.98.
Akichangia, Mbunge wa Moshi Vijijini, Prof. Patrick Ndakidemi, ameipongeza Wizara, taasisi zake za uhifadhi, na wadau wa utalii kwa kazi kubwa ya kuitangaza nchi kimataifa na hivyo kuchangia ongezeko hilo la watalii.
“Tuendelee na mpango wa kutangaza vivutio vya utalii katika nchi za Uarabuni, Japan, Ufaransa, India, na Australia. Ikiwezekana, tutengeneze filamu za utalii kwa lugha za nchi hizo. Tuzitumie pia mashirika ya ndege, vyombo vya habari vya kimataifa, ligi maarufu za mpira duniani, na watu maarufu duniani kutangaza vivutio vyetu. Pia tuendelee kushiriki katika maonesho ya kimataifa kama ITB, ITN ya Ufaransa, na EAC Tourism Expo,” amesema Prof. Ndakidemi.
Naye, Mbunge wa Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Mnzava, ameshauri Serikali kuzipa taasisi za uhifadhi uwezo wa kukusanya mapato yatokanayo na utalii na uhifadhi ili kusaidia kuboresha miundombinu ya utalii, kujenga vituo vya askari, na kuweka uzio wa umeme kwenye mipaka ya hifadhi na kupunguza migogoro kati ya wanyamapori na wananchi.
Mbunge wa Kyerwa, Mhe. Innocent Bilakwate ameipongeza TANAPA na NCAA kwa kusimamia uhifadhi na utalii kwa mafanikio, huku akisisitiza kuwa shughuli za kutangaza utalii ziwe endelevu. Alihimiza matumizi ya programu za livestreaming na kuimarisha kituo cha matangazo ya kidijitali kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Kwa upande wake, Mbunge wa Hai, Mhe. Saashisha Mafue, ameiomba Serikali kuendeleza jitihada za kuainisha vivutio vya utalii wa miamba (Geoparks), hatua itakayoongeza bidhaa za utalii na kusaidia kusambaza wageni katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Mbunge wa Moshi Mjini, Mhe. Priscus Tarimo, ameeleza kuwa Serikali imefanya kazi kubwa kuboresha barabara ya Loduare hadi Golini katika Hifadhi ya Ngorongoro. Alishauri Serikali kuimarisha zaidi barabara za ndani (feeder roads) katika hifadhi ili kurahisisha upatikanaji wa vivutio vilivyotawanyika maeneo mbalimbali.
Wabunge wameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa jitihada kubwa za kutangaza vivutio vya utalii, ambazo zimesaidia kuongeza idadi ya watalii wa kimataifa kutoka 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia 2,141,895 mwaka 2024, huku watalii wa ndani wakiongezeka kutoka 788,933 hadi 3,218,352 katika kipindi hicho.
Kwa upande wa maduhuli ya Serikali yametajwa kuongezeka kutoka Shilingi bilioni 397.42 Mwaka 2020/2021 hadi Shilingi bilioni 901.08 Mwaka 2023/2024. Aidha mwaka wa Fedha 2024/2025 kuanzia Julai 2024, hadi kufikia Aprili 2025, Wizara imekusanya jumla ya Shilingi bilioni 912.90 sawa na asilimia 94.2 ya lengo la makusanyo, kiwango ambacho ni kikubwa kuliko wakati wowote kuwahi kupatikana katika historia ya sekta hii
Pongezi hizo zimetolewa wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii 2025/26 iliyowasilishwa na Waziri Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana, ambaye ameomba Bunge liidhinishe Sh. bilioni 359.98.
Akichangia, Mbunge wa Moshi Vijijini, Prof. Patrick Ndakidemi, ameipongeza Wizara, taasisi zake za uhifadhi, na wadau wa utalii kwa kazi kubwa ya kuitangaza nchi kimataifa na hivyo kuchangia ongezeko hilo la watalii.
“Tuendelee na mpango wa kutangaza vivutio vya utalii katika nchi za Uarabuni, Japan, Ufaransa, India, na Australia. Ikiwezekana, tutengeneze filamu za utalii kwa lugha za nchi hizo. Tuzitumie pia mashirika ya ndege, vyombo vya habari vya kimataifa, ligi maarufu za mpira duniani, na watu maarufu duniani kutangaza vivutio vyetu. Pia tuendelee kushiriki katika maonesho ya kimataifa kama ITB, ITN ya Ufaransa, na EAC Tourism Expo,” amesema Prof. Ndakidemi.
Naye, Mbunge wa Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Mnzava, ameshauri Serikali kuzipa taasisi za uhifadhi uwezo wa kukusanya mapato yatokanayo na utalii na uhifadhi ili kusaidia kuboresha miundombinu ya utalii, kujenga vituo vya askari, na kuweka uzio wa umeme kwenye mipaka ya hifadhi na kupunguza migogoro kati ya wanyamapori na wananchi.
Mbunge wa Kyerwa, Mhe. Innocent Bilakwate ameipongeza TANAPA na NCAA kwa kusimamia uhifadhi na utalii kwa mafanikio, huku akisisitiza kuwa shughuli za kutangaza utalii ziwe endelevu. Alihimiza matumizi ya programu za livestreaming na kuimarisha kituo cha matangazo ya kidijitali kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Kwa upande wake, Mbunge wa Hai, Mhe. Saashisha Mafue, ameiomba Serikali kuendeleza jitihada za kuainisha vivutio vya utalii wa miamba (Geoparks), hatua itakayoongeza bidhaa za utalii na kusaidia kusambaza wageni katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Mbunge wa Moshi Mjini, Mhe. Priscus Tarimo, ameeleza kuwa Serikali imefanya kazi kubwa kuboresha barabara ya Loduare hadi Golini katika Hifadhi ya Ngorongoro. Alishauri Serikali kuimarisha zaidi barabara za ndani (feeder roads) katika hifadhi ili kurahisisha upatikanaji wa vivutio vilivyotawanyika maeneo mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...