Na Mwandishi Wetu - Rufiji


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI na aliyekuwa Mbunge wa Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Juni 30, amejitokeza kuomba ridhaa kwa Chama chake- Chama cha Mapinduzi (CCM) kuchaguliwa kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.

Mhe. Mchengerwa amefika kwenye ofisi ya Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rufiji katika Mji wa Utete kilomita takribani 60 kutoka barabara kuu ya Dar es Salaam - Lindi kuchukua na kisha kukabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Rufiji na baada ya kukamilisha taratibu zote akairejesha.
Mhe. Mchengerwa aliambatana na mama yake mzazi, ambapo baada ya kuwasilisha fomu asema ameamua kutumia haki ya kuchagua na kuchaguliwa ili aendelee kuwaletea maendeleo wananchi wa Rufiji na kisha akaondoka.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...