Na Diana Byera,Bukoba.


Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini ametoa msaada wa vifaa vya ujenzi  wa jiko la  wafungwa kwenye  Gereza la Kilimo Rwamurumba vyenye thamani ya shilingi Milioni  1.3

Akizungumza wakati akikabidhi  msaada huo  Rweikiza amebainisha kuwa ameguswa na adha wanayopata wafungwa wakati wa kuandaa chakula chao kwenye jiko lililoharibika hasa nyakati za mvua .

Amesema kuwa taarifa ya ubovu wa jiko hilo aliipokea  kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ambaye ni mkuu wa Wilaya ,Erasto Sima ndipo akachukua uamuzi wa kuwajibika kama kiongozi.

Alitoa wito kwa jamii kujitoa kwani Gereza ni sehemu inayotoa huduma za jamii kama kurekebisha makosa na kuendelea kurekebisha maadili hivyo wadau wa maendeleo  wasijitenge na maeneo kama hayo.

 Mkuu wa wilaya ya Bukoba Erasto Sima amemshukru mbunge huyo kwa kusikia kilio chao huku akiwaomba wananchi kuwakumbuka wafungwa licha ya kuwa serikali ndiyo yenye jukumu la kuwatunza.

"Serikali inashughulikia miradi Mingi,nimefurahishwa na Mbunge huyu alivyosikia kilio hiki kutoka kwangu kama kiongozi ameunga mkono haraka kwa sababu wafungwa walioko Hapa wanatoka kwenye jamii yetu ,wanapaswa kuishi katika mazingira mazuri na wadau tunapaswa kuelewa Hilo"Amesema Sima

Hata hivyo Mkuu wa Gereza hilo Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza Benard Baroga amekiri kupokea vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tatu (1,300,000/=)huku akimshukru kwa kijitoa kwake katika kuboresha jiko la wafungwa.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...