Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Babu ametoa hamasa kwa Wafanyabiashara Mkoani hapo kuendelea kulipa kodi stahiki ili maendeleo ya nchi yazidi kupatikana.

Kauli hiyo ameitoa tarehe 23 Juni, 2025 wakati wa kuanza kwa Kampeni ya utoaji elimu ya kodi ya mlango kwa mlango mkoani hapo yenye lengo la kuhakikisha kwamba wafanyabiashara wanaelimishwa kuhusu kodi, wanatatuliwa kero zao za kikodi na kujengewa mazingira mazuri ya kulipa kodi.

Amesema kuwa, ulipaji kodi unaleta manufaa kwa Taifa kwa kuleta maendeleo mbalimbali nchini katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu ya barabara, afya, elimu bure, maji safi na salama na hivyo waache visingizio vya kushindwa kulipa kodi zao stahiki kwani kutolipa kodi hizo ni dhuluma kwa Serikali.

“Kuna wengine wakorofi hawataki tu kulipa kodi na wanatoa visingizio kuwa hawajui kutumia mifumo ya TRA, lakini bora mmefika kuwaelimisha ili waache visingizio hivyo na hatimaye walipe kodi zao stahiki”, alisema Babu.

Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. James Jilala amewashukuru Walipakodi mkoani hapo wanaoendelea kulipa kodi zao stahiki na kutoa wito kwa wale ambao bado wamekua wagumu katika kulipa kodi zao stahiki wawe wazalendo na walipe kodi.

Ameongeza kuwa, Wafanyabiashara wanapaswa kufanya matumizi sahihi ya mashine za EFD kwa kutoa risiti halali na kuwaonya wafanyabiashara wenye tabia kupitisha bidhaa za magendo kupitia njia zisizo halali kuacha mara moja na kuhakikisha kwamba wanapitisha bidhaa hizo katika njia sahihi. 

“Ili uweze kulipa kodi iliyo sahihi ni lazima utumie vizuri mashine ya EFD, lakini vile vile nchi yetu hii inapakana na nchi jirani ya Kenya, niwaombe wafanyabiashara wenye tabia ya kupitisha bidhaa za magendo kuacha mara moja kupitisha njia zisizo halali na badala yake watumie njia zilizo sahihi”, alisema Jilala.

Baadhi ya wafanyabiashara mkoani hapo wamepongeza kampeni hiyo na kuomba iwe endelevu na wengine wakishauri kuwa Maafisa wa TRA wanapopita inasaidia kuona uhalisia wa biashara wanazofanya na itasaidia katika suala la makadirio ya kodi.

Kempeni ya elimu kwa Mlipakodi ya mlango kwa mlango ni zoezi endelevu ambalo TRA imekua ikiliendesha nchi nzima kwa kuhakikisha kwamba, Wafanyabiashara wanapewa elimu ya kodi na kukumubushwa haki na wajibu wao katika masuala ya kodi ambapo kwa sasa zoezi hilo lipo mkoani Kilimanjaro na Dar Es Salaam.






Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...