Ataeleza utekelezaji wa nchi kuhusu viwango vya kimataifa vya kazi na Ajira 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete amewasili Jijini Geneva Uswisi kushiriki Mkutano wa 113 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) .

Katika Mkutano huo, Mhe. Ridhiwani ataeleza utekelezaji wa nchi kuhusu Viwango vya Kimataifa vya Kazi na Ajira za Kazi na kuungana na nchi wanachama kujajadili utekelezaji wa mpango kazi na bajeti ya uendeshaji wa Shirika hilo kwa mwaka 2026/27.
Kuelekea mkutano huo, Mhe. Ridhiwani tayari ametembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Uswisi na kukutana na Mhe. Balozi Dkt. Abdallah Possi ambaye pia ni Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Jijini Geneva Uswisi na Mhe. Balozi Dkt. Hoyce Temu pamoja na watendaji wa Ubalozi huo. 
 Katika hatua nyingine, ametumia fursa hiyo kumpongeza Balozi kwa kazi nzuri zinazofanywa na Ofisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuandaa namna nchi itakavyoshiriki vema katika mkutano wa ILO.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...