Kampuni ya Gf Trucks & Equipment Ltd imeibuka mshindi wa jumla wa maonyesho ya biashara ya kimataifa  2025 yanayoendelea jijini Dar es salaam.

Kupitia kiwanda chake cha kuunganisha Magari makubwa cha GF Vehicle Assemblers(GFA) kilichopo Kibaha mkoani Pwani

Katika maonesho hayo yalionza rasmi tarehe 28 mwezi wa sita yameshirikisha makampuni mbambali kutoka nje na ndani ya nchi Baadhi ya nchi ni China,Korea,Uturuki na kutoka Ulaya,Pia nchi za ukanda wa afrika ni miongoni mwa washiriki katika maonyesho hayo yaliokutanisha wafanyabiashara mbalimbali.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi ndiye aliyekua mgeni rasmi na kufanikiwa kutembelea mabanda kadhaa kabla ya kuanza kutoa tuzo na zawadi kwa washindi mbali mbali katika maonyesho hayo.

Mwinyi alitembelea banda la kampuni ya GF na kujionea bidhaaa mbalimbali zinazouzwa na kampuni hiyo, ambapo Magari madogo ya Hyundai,Mahindra ni miongoni mwa magari yanayouzwa  katika kampuni hiyo 

Magari makubwa aina  ya FAW na Mashine na Mitambo ya XCMG pia alijionea jinsi michakato ya awali ya uunganishaji wa magari inavyofanya kupitia kiwanda cha kampuni hiyo cha GFA kilichopo Kibaha mkoani Pwani

Pia Mwinyi aliwapongeza GF kwa kuibuka kuwa vinara wa ma maonyesho hayo na  kuwataka wasibweteke na kupanua zaidi katika uwekezaji  na kuwataka wakaribie zanziba alimaliza Mwinyi

Akizungumza mara baada ya kupokea Tuzo hiyo ya ushindi wa jumla Mkurugezi wa kampuni ya GF ,Ali Karmali alisema wao kama GF wanajivuni kuwekeza nchini kama Kiwanda cha kwanza cha kutengeneza magari nah ii yote imetokana  na mazingira mazuri ya Serikali kwa wawekezaji hivyo tunajivunia kuwa waongoza njia na makampuni mengine yajifunze kwetu  akizungumzia kuhusu kiwanda hicho cha kuunganisha magari alisema wapo katika awamu ya tatu ya upanuzi itakayochukua zaidi ya wafanyakazi 3000 hivo kuongeza ajira kwa watanzania 

Pia aliutoa ushindi huo kwa wafanyakazi kwani bila wao wasingeweza kufanikiwa,GF ni wauzaji wa Magari makubwa ya FWA,XCMG,HYUNDAI  na mitambo ya kutengenezea barabara na sdhunguli za uchimbaji wa madini XCMG.

Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi akimkabidhi Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuunganisha na kutengeneza magari nchini  ya GFA, Ali Karmal tuzo ya mshindi wa jumla wa maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa, jijini Dar es Salaam

Rais wa Zazibar ,Hussen mwinyi akimsikiliza mkurugenzi wa GF ,Ali Karmal wakati alipotembelea banda la kampuni ya GF kwenye maonyesho ya sabasaba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...