Kupitia Program ya BOOST, Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha, imepokea jumla ya Sh. Bilioni 2 na milioni 71 ambayo imewezesha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya Elimu ya Awali na Msingi.
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Zainabu Makwinya kati ya fedha hizo Sh. Milioni 332 zinawezesha ujenzi wa Shule ya Msingi kwenye Shule ya Sekondari, ikiwa ni miongoni mwa Shule zinazojengwa nchi nzima kuwezesha utekelezaji wa Sera ya Elimu, kwa kuzingatia Elimu ya lazima sasa ni miaka kumi.
“Shule hii si tu kwamba itakuwa ya mfano bali inawakilisha taswira ya elimu na ujuzi unaohitaji kulingana na mahitaji ya Karne ya 21 na kufungua fursa kwa kizazi kijacho,” amesema.
Amesisitiza kuwa Serikali ya Tanzania imedhamiria Kuboresha miundombinu ya kimkakati kuwezesha vijana kuwa na maarifa na stadi zitakazowawezesha kujiajiri na kuajiriwa katika nyanja mbalimbali Kitaifa na Kimataifa.
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Zainabu Makwinya kati ya fedha hizo Sh. Milioni 332 zinawezesha ujenzi wa Shule ya Msingi kwenye Shule ya Sekondari, ikiwa ni miongoni mwa Shule zinazojengwa nchi nzima kuwezesha utekelezaji wa Sera ya Elimu, kwa kuzingatia Elimu ya lazima sasa ni miaka kumi.
“Shule hii si tu kwamba itakuwa ya mfano bali inawakilisha taswira ya elimu na ujuzi unaohitaji kulingana na mahitaji ya Karne ya 21 na kufungua fursa kwa kizazi kijacho,” amesema.
Amesisitiza kuwa Serikali ya Tanzania imedhamiria Kuboresha miundombinu ya kimkakati kuwezesha vijana kuwa na maarifa na stadi zitakazowawezesha kujiajiri na kuajiriwa katika nyanja mbalimbali Kitaifa na Kimataifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...