
MKUU wa Wilaya ya Kaliua, Dk. Garald Mongela, amewaongoza maelfu ya wananchi wa wilaya hiyo kushiriki uzinduzi wa miradi ya kimkakati iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru.
Katika mwaka huu Mwenge wa Uhuru umezindua, umeweka mawe ya msingi
na umetembelea miradi tisa ya maendeleo yenye thamani ya Shilingi
2,275,516,058.60.
Miradi hiyo ni uzinduzi wa Klabu ya Wapinga Rushwa Shule ya
Sekondari Mwongozo, Ujenzi wa Nyumba ya Walimu ya Familia Mbili (Two in One) Shule ya Msingi Dk. Charles Msonde Shilingi 110,000,000 na Ujenzi wa Kitakasa Mikono Shule ya Msingi Dk. Charles Msonde Shilingi 10,205,313.
Miradi mingine ni Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD) Zahanati ya Usigala Shilingi 72,400,000, Ujenzi wa Shule ya Sekondari Makingi
Shilingi 603,890,563 na Mtambo wa Kutengeneza Barabara (Motor Grader) Shilingi 1,227,000,000.
Miradi mingine iliyozinduliwa ni Barabara ya Kuelekea Kituo cha Afya Ulyankulu (km. 2) Shilingi 1,603,040.00, Mradi wa Maji Kijiji cha Ulindwanoni Shilingi 219,817,142.60 na Mradi wa Kikundi cha Bodaboda (Boma Road) Shilingi 30,600,000.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...