

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amefanya ukaguzi wa maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika tarehe 25 Julai, 2025 katika Uwanja wa Mashujaa, Mtumba Jijini Dodoma.

Mhe. Nderiananga ametembelea Uwanja huo leo tarehe 22 Julai, 2025 ili kujionea maandalizi ambapo amesema yamefikia hatua nzuri inayoridhisha.


Aidha katika maadhimisho hayo mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...