Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imeshiriki zoezi la ukaguzi na majaribio ya mtambo utakaotumika kuchimba visima vitatu vya gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay Mkoani Mtwara.
Ukaguzi huo uliofanyikia katika Jimbo la Tianjin nchini China, ulilenga kuhakiki uimara na ufanisi wa mtambo huo kabla ya kusafirishwa kuja nchini Tanzania kwa kazi ya uchimbaji wa visima vya gesi asilia inayotarajiwa kuanza Novemba 2025.
Pamoja na ukaguzi wa mtambo huo wenye uwezo wa kuchimba hadi urefu wa mita 8000, PURA pia ilishiriki kama muangalizi katika ukaguzi na majaribio ya mifumo mbalimbali iliyopo katika mtambo huo na mabomba yatakayotumika wakati wa uchimbaji.
Hatua hii ya ukaguzi ni muhimu kwa kuwa hutoa hakikisho la ufanisi wa mtambo kabla ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi.
PURA, kama mdhibiti wa shughuli za mkondo wa juu wa petroli nchini inashiriki na kusimamia hatua zote za mradi kuhakikisha mradi unatekelezwa kama ulivyopangwa.
Inatarajiwa kuwa, visima vitakavyochimbwa (MS-2, MB-5 na Kasa-1x), vitaongeza uzalishaji wa gesi asilia kwa zaidi ya futi za ujazo milioni 30 kwa siku.

Ukaguzi huo uliofanyikia katika Jimbo la Tianjin nchini China, ulilenga kuhakiki uimara na ufanisi wa mtambo huo kabla ya kusafirishwa kuja nchini Tanzania kwa kazi ya uchimbaji wa visima vya gesi asilia inayotarajiwa kuanza Novemba 2025.
Pamoja na ukaguzi wa mtambo huo wenye uwezo wa kuchimba hadi urefu wa mita 8000, PURA pia ilishiriki kama muangalizi katika ukaguzi na majaribio ya mifumo mbalimbali iliyopo katika mtambo huo na mabomba yatakayotumika wakati wa uchimbaji.
Hatua hii ya ukaguzi ni muhimu kwa kuwa hutoa hakikisho la ufanisi wa mtambo kabla ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi.
PURA, kama mdhibiti wa shughuli za mkondo wa juu wa petroli nchini inashiriki na kusimamia hatua zote za mradi kuhakikisha mradi unatekelezwa kama ulivyopangwa.
Inatarajiwa kuwa, visima vitakavyochimbwa (MS-2, MB-5 na Kasa-1x), vitaongeza uzalishaji wa gesi asilia kwa zaidi ya futi za ujazo milioni 30 kwa siku.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...