Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira leo Tarehe 21 Julai, 2025 amefungua mafunzo kwa Watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo wa Mikoa ya Rukwa na Katavi katika Ukumbi uliopo katika Ofisi za Mkuu wa mkoa wa Rukwa.

Mhe.Rwebangira amewasisitiza Watendaji hao kufuatilia mafunzo hayo kwa umakini ili waweze kuelewa kila kinachofundishwa na kutekeleza majukumu yajayo ya Uchaguzi Mkuu wa Ufasaha na weledi.

Mafunzo haya ya siku tatu ambayo yameanza leo tarehe 21 Julai, 2025 yanajumuisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mkoa, Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi na Maafisa Ununuzi.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...