Timu ya Kitaifa ya Wataalam ya kuandaa Mpango wa Pili wa Maboresho ya Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI II) ipo mkoani Mwanza kupata maoni ya wadau kuhusu changamoto zinazokwamisha biashara na uwekezaji nchini.
Lengo ni kupata taarifa zitakazosaidia kuandaa MKUMBI II. Utekelezaji wa MKUMBI II unatarajiwa kuongeza kasi katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuleta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali ambazo zitaibuliwa na sekta binafsi.
Aidha, unatarajiwa utachochea uwekezaji wa sekta binafsi kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2050 unalenga kuwa na uchumi wa thamani ya Dola Trilioni 1 ifikapo 2050. Huku sekta binafsi ikitarajiwa kuchangia kwa asilimia 65 na kutoa ajira kwa asilimia 85.








Lengo ni kupata taarifa zitakazosaidia kuandaa MKUMBI II. Utekelezaji wa MKUMBI II unatarajiwa kuongeza kasi katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuleta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali ambazo zitaibuliwa na sekta binafsi.
Aidha, unatarajiwa utachochea uwekezaji wa sekta binafsi kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2050 unalenga kuwa na uchumi wa thamani ya Dola Trilioni 1 ifikapo 2050. Huku sekta binafsi ikitarajiwa kuchangia kwa asilimia 65 na kutoa ajira kwa asilimia 85.









Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...