Sajenti Emmanuel Kisiri ambae ni polisi kata wa kata ya Ikoma Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara ameendelea kuihimiza jamii kulinda maadili ya watoto

Akiendelea na kampeni yake ya Nyumba kwa Nyumba katika kijiji cha Robanda kitongoji cha Momorogoro kata ya Ikoma Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara Sajenti Emmanuel aliwakumbusha wazazi na walezi mambo yafutayo:

Kumchapa mtoto viboko vichache ni kumfundisha mtoto tofauti ya jema na baya huku wakitumia lugha ya upendo kwa kumweleza mtoto kwa upole juu ya makosa yake

Wazazi kutenga mda wa kuzungumza na watoto wao kila siku na pia kuwapa nafasi ya kuongea bila kumkataza mtoto huku ukimuonyesha mtoto kwamba hisia zake ni muhimu

Na mwisho aliwakumbusha wazazi kua michezo mbalimbali kwa mtoto si kupoteza muda ni njia ya mtoto kujifunza, kujenga ubunifu, na kuendeleza uhusiano mzuri na wenzake ivyo basi aliwasihii wazazi kuwaruhusu watoto kucheze ila wakiwa kwenye uangalizi wao ili watoto waufurahie utoto wao.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...